2 Samuel 23

Maneno Ya Mwisho Ya Daudi

1 aHaya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese,
neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana,
mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo,
mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:


2 b“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu,
neno lake lilikuwa ulimini mwangu.

3 cMungu wa Israeli alinena,
mwamba wa Israeli akaniambia:
‘Mtu anatawala watu kwa haki,
wakati anapotawala
akiwa na hofu ya Mungu,

4 dyeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo
asubuhi isiyo na mawingu,
kama mwanga baada ya mvua
uchipuzao majani kutoka ardhini.’


5 e“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu
mbele za Mungu?
Je, hajafanya Agano la milele nami,
lililopangwa na kuimarishwa
kila sehemu?
Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu
na kunijalia matakwa yangu yote?

6 fLakini watu waovu wote
watatupwa kando kama miiba,
ambayo haikusanywi kwa mkono.

7 Yeyote agusaye miiba
hutumia chombo cha chuma
au mpini wa mkuki,
nayo huchomwa pale ilipo.”

Mashujaa Wa Daudi

(1 Nyakati 11:10-41)

8 gHaya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi:

Yosheb-Bashebethi,
Yosheb-Bashebethi au Yashobeamu ( 1Nya 11:11 ).
Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.

9 iWa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai,
Dodai tafsiri nyingine zinamwita Dodo.
Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.

11Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia. 12Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.

13 kWakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai. 14 lWakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu. 15Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!” 16 mBasi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana. 17 n oAkasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa.

Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.

18 pAbishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu. 19Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.

20 qBenaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba. 21 rPia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe. 22Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu. 23 sYeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.


24 tMiongoni mwa wale Thelathini walikuwepo:
Asaheli ndugu wa Yoabu;
Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;

25 uShama, Mharodi;
Elika, Mharodi;

26 vHelesi, Mpalti;
Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;

27 Abiezeri kutoka Anathothi;
Mebunai, Mhushathi;

28 wSalmoni, Mwahohi;
Maharai, Mnetofathi;

29 xHeledi mwana wa Baana, Mnetofathi;
Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;

30 yBenaya Mpirathoni;
Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;

31 zAbi-Alboni, Mwaribathi;
Azmawethi, Mbarhumi;

32 Eliaba, Mshaalboni;
wana wa Yasheni;
Yonathani
33mwana wa Shama, Mharari;
Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;

34 aaElifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi;
Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;

35 abHezro, Mkarmeli;
Paarai, Mwarbi;

36 acIgali mwana wa Nathani kutoka Soba;
Bani, Mgadi;

37 adSeleki, Mwamoni;
Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;

38 aeIra, Mwithiri;
Garebu, Mwithiri;

39 afna Uria, Mhiti.
Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.
Copyright information for SwhKC